• Afisa Masuuli na mtendaji mkuu wa serikali ya kijiji;
• Kusimamia ulinzi na usalama wa raia na mali zao, kuwa mlinzi wa amani na msimamizi wa utawala bora katika kijiji;
• Kuratibu na kusimamia upangaji wa mipango ya maendeleo ya kijiji;
• Katibu wa mikutano na kamati zote za Halmashauri ya kijiji;
• Kutafsiri na Kusimamia Sera, Sheria na Taratibu;
• Kuandaa taarifa ya utekelezaji wa kazi katika eneo lake na kuhamasisha wananchi katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya kuondoa njaa, umaskini na kuongeza uzalishaji mali;
• Kiongozi wa wakuu wa vitengo vya klitaalam katika kijiji;
• Kusimamia, kukusanya na kuhifadhi kumbukumbu zote na nyaraka za kijiji;
• Mwenyekiti wa kikao cha wataalam waliopo katika kijiji;
• Kupokea, kusikiliza na kutatua malalamiko na migogoro ya wananchi;
• Kusimamia utungaji wa Sheria Ndogo za kijiji; na
• Atawajibika kwa Mtendaji Mkuu wa Kata.
• Kuajiriwa mwenye Elimu ya kidato cha Nne(IV) au Sita (VI) aliyehitimu mafunzo ya Astashahada/Cheti katika moja ya fani zifuatazo: Utawala,Sheria, Elimu ya Jamii, Usimamizi wa Fedha, Maendeleo ya Jamii na Sayansi ya Sanaa kutoka Chuo Cha Serikali za Mitaa Hombolo, Dodoma au Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.